Paulo anawambia Warumi katika (Warumi 8: 18) kuwa "kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama utukufu ule utakaofunuliwa kwetu" kwa hiyo mateso ambayo Mkristo unayapitia leo ni mepesi kulinganisha na utukufu utakaofunuliwa kwetu siku ya mwisho .
Mateso tunayopitia sasa ni ya kitambo kidogo tu. Tukivumilia hadi mwisho kuna utukufu mwingi wa milele utakaofunuliwa siku ya mwisho. Tukivumilia hadi mwisho kuna utukufu mwingi wa milele utakaofunuliwa siku ile ya
mwisho.
Biblia inasema katika kitabu cha Wakorintho ( 2 wakorintho 4: 17) "maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda tu , hutufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana"
MATESO YETU NI YA KITAMBO KIDOGO TU
Maandiko yafuatayo yanafafanua eneo hili:-
ZABURI 30 : 5 inasema " Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo katika radhi yake mna uhai . Huenda kilio huja kukaa usiku , lakini asubuhi huja furaha " ISAYA 54 : 7-8 " Kwa kitambo kidogo nimekuacha , lakini kwa rehema nyingi nitakukusanya. Kwa ghadhabu ifurikayo nalikuficha uso wangu kwa kitambo , lakini kwa fadhili za milele nitakurehemu asema BWANA mkombozi wako" YOHANA 16: 20 "amini amini nawambia, ninyi mtalia na kuomboleza, bali ulimwengu utafurahi, ninyi mtahuzunishwa lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha".
1 PETRO 1: 6 "mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo , ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali" 1PETRO 5: 10 " Na MUNGU wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika KRISTO , mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu"
Inawezekana unapitia mateso kama mkristo na watu wengine wananong'ona kuwa mateso uliyonayo ni kutokana na dhambi. Usikate tamaa kwa kuwa BWANA hajakusahau wala kukuacha , kuna furaha inakuja asubuhi. Mungu atakuthibitisha na kukutia nguvu.
MATESO HUISHIA KATIKA FURAHA NA BARAKA
AYUBU 5: 17 "Tazama yu heri mtu yule MUNGU amwadhibuye; kwa hiyo usidharau kurudiwa na huyo mwenyezi " Yakobo 5: 11 "Angalieni twaita heri waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake AYUBU, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma " ISAYA 61 : 2-3 " kutangaza mwaka wa BWANA uliokubaliwa na siku ya kisasi cha MUNGU wetu ; kuwafariji wote waliao. Kuwaagiza hao walio katika Sayuni wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito, wapate kuitwa miti ya haki iliyopandwa na BWANA ili atukuzwe."
1Petro 4: 13 " Lakini kama mnavyoshiriki mateso ya Kristo, furahini ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe."
MATESO HUDHIHIRISHA UPENDO NA UAMINIFU WA MUNGU KWETU.
Kumbukumbu la Torati 8: 5 " Nawe fikiri moyoni mwako ya kuwa kama vile Baba amrudivyo mwanawe ndivyo BWANA MUNGU WAKO akurudivyo " ZABURI 119 : 75 "Najua kuwa hukumu zako ni za haki Ee Bwana, na kwa uaminifu umenitesa" Mithali 3: 12 " Kwa kuwa BWANA ampendaye humrudi, kama vile baba mwanaye ampendezaye" WAKORINTHO 11: 32 " Ila tuhukumiwapo, twarudiwa na Bwana, isijeikatupasa adhabu pamoja na dunia" Ufunuo 3: 19 "Wote niwapendao mimi nawakemea na kuwarudi , basi uwe na bidii ukatubu."
HITIMISHO.
MUNGU awatendea kama wana, maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye? " ZABURI 34 : 19 " Mateso ya mwenye haki ni mengi lakini BWANA humponya nayo yote."
Related Posts:
SERIKALI YAPINGA UTARATIBU WA AJIRA ZA MIKATABA
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, George Mkuchika amesema kuwa, ofisi yake haiungi mkono
mfumo wa kazi kwa mikataba.
Waziri Mkuchika ameongeza kuwa, mfumo huo ni gharama
kubwa ukilinganish… Read More
POLISI ACHINJA MPENZI WAKE KISHA NAYE KUJIPIGA RISASI AKIMTUHUMU KUWA NA MICHEPUKO HUKO SONGWE
Taarifa kutoka Momba mkoani Songwe
zinaeleza kwamba askari polisi wa kitengo cha usalama barabarani mwanaume
ambaye jina lake halijawekwa wazi mwenye umri wa miaka 29 anadaiwa
kumuua mpenzi wake kwa… Read More
Women of Jerusalem Warned
Isaiah 33:9-20
Rise up, ye women that are at ease ; hear my voice, ye careless daughters ; give ear unto my speech. Many days and years shall ye be troubled, ye careless women : for the vintage shall fail, the gathering… Read More
Jacob Blesses Ephraim and Manasseh
GENESIS 48:1-22
And it came to pass after these things, that one told Joseph, Behold, thy father is sick : and he took with him his two sons, Manasseh and Ephraim. And one told Jacob, and said, Behold, thy son Joseph… Read More
Zifahamu faida za kulia
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});
Mtafiti wa machozi Bergman anasema, "Kuzuia machozi huongeza viwango
vya shida, na huchangia magonjwa yaliyotokana na matatizo, kama
shinikizo la damu, matatiz… Read More
0 comments:
Post a Comment