IMANI haitegemei  matendo , bali matendo ni matokeo ya imani

Ukiweka kwa namna nyingine ni kwamba  tunachokiamni hakitokani na kile tunachofanya, bali tunafanya kutokana na kile tunachokiamini

Wokovu hautokani na matendo , bali hutokana na imani.

IMANI ILETAYO WOKOVU

  • Waefeso 2:8-9 “ kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani ambayo hiyo haijatokana na nafsi  zenu, ni kipawa cha Mungu , wala si kwa matendo mtu awaye yote asije akajisifu”

  • Neema ya Mungu iletayo wokovu huja kwa njia ya imani

  • Tunaposikia Neno la Mungu, mioyo yetu hufunguka  na imani huingia na kutujenga.

  • Hatuwezi kujidai katika imani kwa sababu Mungu ametupa tulipofungua mioyo yetu kusikia injili.

Warumi 4: 4-5 “ Lakini kwa mtu afanyaye kazi, ujira wake hauhesabiwi kuwa ni neema, bali kuwa ni deni .Lakini kwa mtu asiyefanya kazi ,bali atamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiyekuwa mtauwa, imani yake mtu huyo imehesabiwa kuwa haki”

  • Kwa hiyo ili tupokee haki ni lazima tuwe na imani

  • Imani katika Yesu Kristo itokanayo na kusikia injili , hutolewa kwetu na Mungu mwenye haki. Waebrania 11: 6 “ maana pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu. Maana kila amwendeaye yeye ni lazima aamini kuwa yeye yupo, naye huwapa thawabu wale wamfuatao.”

  • Hakuna mwanadamu awezaye kumpendeza Mungu pasipo na Imani.

  • Hakuna mtu awezaye kumwendea Mungu pasipo imani

  • Hakuna mtu awezaye kupokea wokovu pasipo kuwa na imani itokanayo na kusikia neon la Mungu.


MFANO KATIKA BIBLIA

Kulikuwa na mtu jina lake ni Nikodemu aliyekuwa mtawala wa Wayahudi Nyakati za Yesu. Mtu alimwendea Yesu kwa siri usiku, akamuliza Yesu nifanye nini ili niweze kuurithi ufalme wa MUngu? Yesu akajibu na kusema (Yohana 3:3) “ Hakika hakika nakwambia mtu asipozaliwa mara ya pili  hawezi kuuona ufalme wa Mungu” Nikodemo alitaka kujua jinsi gani inavyowezekana kuzaliwa mara ya pili , akijua kwamba yeye ni mzee.

Yohana  3: 16-18 “ Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwana wake wa pekee ili kila mtu aaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma mwana ili ahukumu ulimwengu bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi , asiye amini amekwisha hukumiwa kwa sababu hakuliamini jina pekee la Mwana wa Mungu.” Warumi  10 :9-10

JE TUKIAMINI KITU GANI?

Tunahitaji kumwamini  Yesu ndani yetu ,aliye kufa kwa ajili ya dhambi zetu , alizikwa na siku ya tatu alifufuka katika wafu. Biblia inasema tukiamini na kukuiri kwa vinywa vyetu tutaokoka.

Mungu atatupa haki yake kwa neema. Sasa tutazaliwa mara ya pili kwa Roho Mtakatifu

IMANI INAWEZA KUTUMIKA WAPI?

  • Imani hutumika katika hali zote za maisha

  • Katika wokovu (Waefeso 2: 8) Galatia  3: 11

  • Kwenye maombi – 1Yohana 5: 14-15

  • Maeneo ya Uchumi na fedha – Wafilipi  4: 19

  • Kwenye chakula – Warumi  14 : 23

  • Kupata usingizi mtamu – Zaburi -127: 2; Zaburi  3 : 4-8

Related Posts:

  • The God of Victory and Judgment  Psalm 76:1-12 In Judah is God known : his name is great in Israel. In Salem also is his tabernacle, and his dwelling place in Zion. There brake he the arrows of the bow, the shield, and the sword, and the battle. Se… Read More
  • The Promise of God’s Grace to Israel  Isaiah 30:18-26 And therefore will the Lord wait, that he may be gracious unto you, and therefore will he be exalted, that he may have mercy upon you : for the Lord is a God of judgment : blessed are all they that wa… Read More
  • The Prayer of an Old Man Psalm 71:1-24 (adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({}); In thee, O Lord, do I put my trust : let me never be put to confusion. Deliver me in thy righteousness, and cause me to escape : incline thine ear unto … Read More
  • Serikali kukopesha vijana Pikipiki Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Ally Hapi ametangaza na kutoa agizo kwa viongozi wa Halmshauri ya Kinondoni kuanza kutoa mikopo ya vitendea kazi kwa vijana mbalimbali wilayani huo zikiwemo Pikipiki ili vijana waweze kuj… Read More
  • Zifahamu faida za kulia (adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({}); Mtafiti wa machozi Bergman anasema, "Kuzuia machozi huongeza viwango vya shida, na huchangia magonjwa yaliyotokana na matatizo, kama shinikizo la damu, matatiz… Read More

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive

Popular Posts