IMANI haitegemei
matendo , bali matendo ni matokeo ya imani
Ukiweka kwa namna nyingine ni kwamba tunachokiamni hakitokani na kile
tunachofanya, bali tunafanya kutokana na kile tunachokiamini
Wokovu hautokani na matendo , bali hutokana na imani.
IMANI ILETAYO WOKOVU
Waefeso 2:8-9 “ kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya
imani ambayo hiyo haijatokana na nafsi
zenu, ni kipawa cha Mungu , wala si kwa matendo mtu awaye yote asije
akajisifu”
Neema ya Mungu iletayo wokovu huja kwa njia ya imani
Tunaposikia Neno la Mungu, mioyo yetu hufunguka na imani huingia na kutujenga.
Hatuwezi kujidai katika imani kwa sababu Mungu ametupa
tulipofungua mioyo yetu kusikia injili.
Warumi 4: 4-5 “ Lakini kwa mtu afanyaye kazi, ujira wake
hauhesabiwi kuwa ni neema, bali kuwa ni deni .Lakini kwa mtu asiyefanya kazi
,bali atamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiyekuwa mtauwa, imani yake mtu
huyo imehesabiwa kuwa haki”
Kwa hiyo ili tupokee haki ni lazima tuwe na imani
Imani katika Yesu Kristo itokanayo na kusikia injili ,
hutolewa kwetu na Mungu mwenye haki. Waebrania 11: 6 “ maana pasipo imani
haiwezekani kumpendeza Mungu. Maana kila amwendeaye yeye ni lazima aamini kuwa
yeye yupo, naye huwapa thawabu wale wamfuatao.”
Hakuna mwanadamu awezaye kumpendeza Mungu pasipo na Imani.
Hakuna mtu awezaye kumwendea Mungu pasipo imani
Hakuna mtu awezaye kupokea wokovu pasipo kuwa na imani
itokanayo na kusikia neon la Mungu.
MFANO KATIKA BIBLIA
Kulikuwa na mtu jina lake ni Nikodemu aliyekuwa mtawala wa
Wayahudi Nyakati za Yesu. Mtu alimwendea Yesu kwa siri usiku, akamuliza Yesu
nifanye nini ili niweze kuurithi ufalme wa MUngu? Yesu akajibu na kusema
(Yohana 3:3) “ Hakika hakika nakwambia mtu asipozaliwa mara ya pili hawezi kuuona ufalme wa Mungu” Nikodemo
alitaka kujua jinsi gani inavyowezekana kuzaliwa mara ya pili , akijua kwamba
yeye ni mzee.
Yohana 3: 16-18 “ Kwa
maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwana wake wa pekee ili
kila mtu aaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma
mwana ili ahukumu ulimwengu bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye
yeye hahukumiwi , asiye amini amekwisha hukumiwa kwa sababu hakuliamini jina
pekee la Mwana wa Mungu.” Warumi 10 :9-10
JE TUKIAMINI KITU GANI?
Tunahitaji kumwamini
Yesu ndani yetu ,aliye kufa kwa ajili ya dhambi zetu , alizikwa na siku
ya tatu alifufuka katika wafu. Biblia inasema tukiamini na kukuiri kwa vinywa
vyetu tutaokoka.
Mungu atatupa haki yake kwa neema. Sasa tutazaliwa mara ya
pili kwa Roho Mtakatifu
IMANI INAWEZA KUTUMIKA WAPI?
Imani hutumika katika hali zote za maisha
Katika wokovu (Waefeso 2: 8) Galatia 3: 11
Kwenye maombi – 1Yohana 5: 14-15
Maeneo ya Uchumi na fedha – Wafilipi 4: 19
Kwenye chakula – Warumi 14 : 23
Kupata usingizi mtamu – Zaburi -127: 2; Zaburi 3 : 4-8
0 comments:
Post a Comment