UBATIZO NI NI?

Ubatizo ni neno la Kigiriki ‘Baptizo’ lenye  kumanisha :-

  • Kuchovya ( to dip)

  • Kuzamisha ( to submerge)

  • Kugharikisha( to overwhelm)

  • Kufunika kabisa kwa kimiminika

  • Kuchovya kitu katika kimiminika na kukitoa tena nje 

     

HATUA ZA MKRISTO ILI KUBATIZWA UBATIZO WA MAJI MENGI

Toba : Matendo ya Mitume 2: 37 -38

Ni lazima toba ifanyike kabla ya kubatizwa ubatizo wa maji mengi. Maana ubatizo ni ishara ya nje inayodhihirisha badiliko la ndani lililofanyika katika moyo kupitia toba. Ubatizo pasipo badiliko la ndani na mahusiano mapya na Mungu hauna tija.

Ni lazima kuamini : Mark  16: 15- 16 , Matendo 8: 36- 39

Ni pale tu tunapomwamini  Yesu Kristo mwana wa Mungu ndipo tubatizwe ubatizo wa maji mengi .Tunaona Philipo na Towashi , ni pale tu Towashi alipomwamini Yesu ndipo waliposhuka majini na kubatizwa , tazama Biblia inasema tena wakapanda kutoka majini.

Ni lazima kuwa na ufahamu au nia njema ndani yako. 1Petro 3:21

Ni lazima kukubali kuwa mwanafunzi wa Yesu .Mathayo 28 : 19- 20 “Basi enendeni mkawafanye mataifa  yote kuwa wanafunzi wangu, mkiwabatiza kwa jina la Baba la Mwana na Roho Mtakatifu, na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi, na tazama mimi nipo pamoja nanyi siku zote hata ukamilifu wa dahari.”

FAIDA ZA KIROHO ZA UBATIZO WA MAJI MENGI

Kuelewa umuhimu wa kiroho  kubatizwa  ubatizo wa maji mengi  soma Warumi  6: 3-7, Wakolosai  2: 12

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive

Popular Posts